Academia.eduAcademia.edu

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ______________ KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE

44.-(1)

Maswali ya nyongeza yanaweza kuulizwa na Mbunge yeyote kwa madhumuni ya kupata ufafanuzi zaidi juu ya jambo lolote lililotajwa katika jibu lililotolewa.

(2) Mbunge anayeuliza swali la msingi ataruhusiwa kuuliza maswali ya nyongeza yasiyozidi mawili na Mbunge mwingine yeyote atakayepewa nafasi ataruhusiwa kuuliza swali moja tu la nyongeza.

(3) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, swali ambalo litawekwa katika vifungu vya (a) na (b) litahesabiwa kuwa ni maswali mawili.

(4) Isipokuwa kama Spika ataelekeza vinginevyo, Wabunge watakaouliza maswali ya nyongeza hawatazidi watatu kwa swali moja la msingi, na Mbunge hataruhusiwa kusoma swali lake. (2) Endapo Spika atakataa swali la nyongeza kwa kukiuka masharti ya Kanuni hizi, swali hilo halitajibiwa wala halitaoneshwa kwenye Taarifa Rasmi. (3) Iwapo Spika ataridhika kuwa, swali la msingi aul nyongeza halijapata majibu ya kuridhisha, ataaiza lijibiwe kwa ufasaha zaidi katika kikao kingine cha Bunge.

46.-(1) Waziri anayeulizwa swali atakuwa na wajibu wa kulijibu swali hilo kwa ukamilifu kama lilivyoulizwa , isipokuwa kwamba, kama jibu linalohusika ni refu au lina takwimu nyingi, Waziri atampa Mbunge muuliza swali nakala ya jibu mapema baada ya kikao kuanza, kabla ya muda wa kmujibu swali hilo haujafikiwa.

(2) Endapo Mbunge muuliza swali atamwomba Waziri ampatie nakala ya jibu la swali lake kabla ya muda wa kujibu swali hili haujafikiwa basi Waziri anaweza kumpa Mbunge muuliza swali nakala ya jibu kama lilivyoombwa.

(3) Waziri Mkuu au Waziri mwingine yeyote au Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaweza kutoa majibu ya nyongeza kwa majibu yaliyotolewa na Waziri.

47.-(1)

Baada ya Muda wa Maswali kwisha, Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja kuwa Shughuli za Bunge kama zilivyooneshwa kwenye Orodha ya Shughuli ziahirishwe ili Bunge lijadili jambo halisi la dharura na muhimu kwa umma.

(2) Hoja ya namna hiyo itakuwa ni maalumu na inaweza kutolewa wakati wowote hata kama majadiliano yatakuwa yanaendelea.

(3) Hoja itatolewa na Mbunge kwa kusimama mahali pake na kuomba idhini ya Spika kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli za Bunge kwa madhumuni ya kujadili jambo halisi la dharura na muhimu kwa umma.

(4) Iwapo Spika ataridhika kwamba jambo hilo ni la dharura, halisi na lina maslahi kwa umma, basi ataruhusu hoja hiyo itolewe kwa muda usiozidi dakika tano na mjadala juu ya hoja hiyo utaendelea kwa muda ambao Spika ataona unafaa kwa kuzingatia mazingira ya suala linalojadiliwa. (2) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hii litahesabiwa tu kuwa ni jambo halisi, iwapo:-

ni jambo mahususi;

(b) halikuwekwa katika lugha ya jumla mno au lina mambo mengine mchanganyiko;

(c) halikutolewa kwa kutegemea habari zisizo za uhakika au habari halisi juu ya jamo hilo hazipatikani; au (d) halihusu mambo ya kinadharia.

(3) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hii litahesabiwa kuwa ni jambo la dharura, iwapo:-

athari zake ni dhahiri na linaweza kutokea wakati wowote;

(b) limetokea siku hiyo au siku za karibuni na limetwa bila kuchelewa; au (c) hakutatokea fursa ya kulijadili siku za karibuni kwa njia ya kawaida ya kushghulikia mambo ya Bunge.

(4) Jambo lolote litahesabiswa kuwa ni lenye maslahi kwa umma iwapo utatuzi wake unategemea hatua zaidi kuliko zile za utekelezaji wa kawaida wa sheria peke yake.

49.-(1)

Waziri anaweza kutoa kauli Bungeni kuhusu jambo lolote linaloihusu Serikali.

(2) Kauli za aina hiyo zinaweza kutolewa kwa idhini ya Spika katika wakati unaofaa kufuatana na mpangilio wa Shughuli za Bunge na zitahusu jambo mahususi, halisi na zisizozua mjadala na muda wa kusema utakuwa ni dakika zisizozidi thelathini.

(3) Waziri mwenye kutoa kauli atawajibika kutoa nakala ya kauli yake kwa Wabunge wote wakati anapoiwasilisha Bungeni. (3) Endapo Spika ataamua kwamba jambo hilo linahusu haki za Bunge, basi atampa nafasi Mbunge mhusika kutoa hoja yake kisha hoja hiyo itapewa kipaumbele katika kupanga shughuli nyingine zote za kikao kinachohusika. (10) Iwapo Mbunge anapenda kufanya mabadiliko ya maneno aliyoyatumia katika hoja anayokusudia kuitoa, anaweza kufanya hivyo kwa kutoa taarifa ya kutaka kufanya mabadiliko angalau siku moja kabla ya siku ile ambapo hoja hiyo imewekwa kwenye Orodha ya Shughuli ili ijadiliwe.

(11) Mbunge ambaye hakutoa taarifa ya kutaka kufanya marekebisho au mabadiliko katika hoja yake, anaweza kumwomba Spika afanye marekebisho au mabadiliko katika hoja hiyo wakati anawasilisha hoja yake bila ya kutoa taarifa.

(12) Pamoja na kuwa taarifa ya kutaka kufanya marekebisho au mabadiliko itakuwa imetolewa, marekebisho au mabadiliko yoyote hayatakubaliwa kama, kwa maoni ya Spika, mabadiliko hayo yanabadilisha mambo ya msingi yaliyomo katika hoja au yanabadilisha makusudio au upeo wa hoja hiyo.

56.-(1)

Mbunge atakapoitwa na Spika kutoa hoja, atasimama mahali pake na kutoa hoja yake.

(2) Hoja au marekebisho au mabadiliko ya hoja yoyote, yatahitaji kuungwa mkono na Wabunge wasiopungua kumi na endapo hayataungwa mkono hoja au marekebisho au mabadiliko hayo yatatenguka na Katibu ataweka kumbukumbu kwenye Taarifa Rasmi kwamba, kwa kuwa hoja au marekebisho au mabadiliko hayo hayakuungwa mkono, basi hayakujadiliwa.

(3) Mbunge anaweza kuunga mkono hoja kwa kusimama tu mahali pake bila kusema lolote kuhusu hoja hiyo, kisha akakaa; lakini Mbunge aliyefanya hivyo bado atakuwa na haki ya kuizungumzia hoja hiyo hapo baadaye. (2) Kabla ya kutoa hoja hiyo, mtoa hoja atamkabidhi Katibu maandishi yenye saini yake na yanayoonesha mabadiliko anayotaka yafanywe.

(3) Kila badiliko linalopendekezwa sharti liwiane na hoja inayokusudiwa kufanyiwa mabadiliko na pia liungwe mkono na lisiingize jambo lolote ambalo, kwa maoni ya Spika, linaweza kuwasilishwa kwa hoja maalumu.

(4) Badiliko lolote halitaruhusiwa kama, kwa maoni ya Spika, linapingana moja kwa moja na hoja ya msingi iliyotolewa.

(5) Iwapo hoja ya mabadiliko inapendekeza kuondoa maneno fulani na kuingiza maneno mengine, basi mjadala juu ya suala la kufanya mabadiliko unaweza kuangalia kwa pamoja yale maneno yanayopendekezwa yaondolewe na maneno ambayo yanapendekezwa yaingizwe.

(6) Iwapo hoja inapendekeza kuondoa au kuingiza maneno, mjadala utahusu tu uondoaji au uingizaji wa maneno mapya, kadri itakavyokuwa.

(7) Hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja nyingine ya mabadiliko sharti ihusiane na hoja ya kwanza ya mabadiliko na itatolewa, itajadiliwa na kuamuliwa kabla ya ile hoja ya kwanza ya mabadiliko kufanyiwa uamuzi.

58.-(1) Endapo Mbunge anapenda kupendekeza mabadiliko yafanywe katika hoja kwa kufuata masharti ya Kanuni hizi, anaweza kutoa hoja yake ya kufanya mabadiliko wakati wowote baada ya hoja anayotaka kuibadilisha kutolewa, lakini kabla Bunge halijahojiwa liifanyie uamuzi.

(2) Endapo kuna mapendekezo mawili au zaidi ya kubadilisha hoja moja, Spika atawaita watoa hoja hizo kwa kufuata mpangilio atakaoamua.

(3) Iwapo mapendekezo yote ya mabadiliko yameamuliwa, Spika ataitoa tena hoja ya awali ili ijadiliwe kama itakavyokuwa imebadilishwa.

(4) Hoja yoyote inaweza kuondolewa wakati wowote kabla hoja hiyo haijafikishwa Bungeni iwapo Mbunge mtoa hoja atatoa kwa Katibu, taarifa ya maandishi ya kuiondoa hoja hiyo. (2) Isipokuwa kwamba, Mbunge yeyote hataanza kuzungumza hadi aitwe na Spika ama kwa jina au wadhifa wake na kumruhusu kusema na wakati wa kusema ataelekeza maneno yake kwa Spika.

(3) Mbunge akimaliza kutoa maelezo yake atakaa kwenye nafasi yake na hapo Spika atamwita Mbunge mwingine aliyempelekea ombi la maandishi au kama Spika hakupata ombi lolote la maandishi, basi Mbunge mwingine yeyote anayetaka kujadili hoja anaweza kusimama mahali pake na kusubiri Spika amwone.

(4) Iwapo Wabunge wawili au zaidi watasimama wakati mmoja, Spika atamwita Mbunge atakayemwona kwanza. (2) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Kanuni hii, Mbunge anayejadili hoja ataruhusiwa kusema kwa muda unaoruhusiwa na Kanuni hizi.

63.-(1)

Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katiba yanayolinda na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge, ni marufuku kabisa kusema uongo Bungeni na kwa sababu hiyo, Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni ana wajibu wa kuhakikisha kwamba anatoa kauli au maelezo kuhusu jambo au suala ambalo yeye mwenyewe anaamini kuwa ni la kweli na siyo jambo la kubuni au la kubahatisha tu.

(2) Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni hatachukuliwa kuwa anasema uongo iwapo anafanya rejea ya habari kuhusu jambo fulani lililotangazwa au lililoandikwa na vyombo vya habari.

(3) Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama mahali pake na kutamka "kuhusu utaratibu" na baada ya kuruhusiwa na Spika, kudai kwamba, Mbunge aliyekuwa anasema kabla yake ametoa maelezo ya uongo kuhusu jambo au suala alilokuwa analisema Bungeni.

(4) Mbunge anayetoa madai kwa mujibu wa fasili ya (3) ya Kanuni hii atakuwa na wajibu wa kutoa na kuthibitisha ukweli kuhusu jambo au suala hilo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge.

(5) Bila ya kuathiri masharti ya fasili zilizotangulia za Kanuni hii, Spika au Mbunge mwingine yeyote, baada ya kutoa maelezo mafupi ya ushahidi unaotilia mashaka ya dhahiri kuhusu ukweli wa kauli au usemi au maelezo juu ya jambo au suala ambalo Mbunge amelisema Bungeni, anaweza kumdai Mbunge huyo atoe uthibitisho wa ukweli wa kauli au usemi au maelezo yake na kama Kutosema uongo Bungeni atashindwa kufanya hivyo, afute kauli au usemi au maelezo yake hayo.

(6) Mbunge aliyetakiwa kuthibitisha ukweli wa kauli au usemi au maelezo yake aliyoyatoa Bungeni, atawajibika kutoa uthibitisho huo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge, papo hapo au katika muda atakaopewa na Spika kwa ajili ya kufanya hivyo.

(7) Endapo Mbunge aliyetakiwa kuthibitisha kauli au usemi au maelezo yake aliyoyatoa Bungeni atashindwa kufanya hivyo, anaweza kujirekebisha kwa kufuta kauli au usemi au maelezo yake hayo, papo hapo au katika muda atakaokuwa amepewa na Spika kwa ajili ya kuthibitisha kauli au usemi au maelezo yake. ikiwa ni kosa lake la kwanza, asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi;

(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi, asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

(c) achukuliwe hatua nyingine za kinidhamu zitakazotajwa katika hoja yake. (f) hatamsema vibaya au kutoa lugha ya matusi kwa Mbunge au mtu mwingine yeyote;

(g) hatatumia lugha ya kuudhi au inayodhalilisha watu wengine.

(2) Mbunge yeyote anayeamini kuwa Mbunge mwingine amevunja au amekiuka masharti ya fasili ya (1) (2) Mbunge ambaye amezungumza juu ya hoja anaweza kuzungumza tena juu ya hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja aliyoisemea; na Mbunge ambaye amependekeza kufanya mabadiliko katika hoja ya awali, anaweza kuzungumza tena juu ya hoja ya awali baada ya mabadiliko kufanyika.

(3) Mbunge mtoa hoja ya msingi au mtoa hoja ya kutaka kufanya mabadiliko katika hoja iliyokwisha kutolewa, atakuwa na haki ya kujibu kabla uamuzi juu ya hoja hiyo haujatolewa.

Kuzungumza zaidi ya mara moja (4) Wakati wa kujibu, mtoa hoja atapaswa kujibu mambo yale tu yaliyozungumzwa na Wabunge waliochangia hoja yake na hataruhusiwa kutoa maelezo yoyote mapya, isipokuwa kama maelezo hayo ni ya lazima kwa madhumuni ya kufafanua jambo lililochangiwa na Wabunge.

(5) Mbunge yeyote hataruhusiwa kusema Bungeni baada ya Spika kuwahoji Wabunge na kura ya sauti ama ya elektroniki au ya siri ya "ndiyo" au "siyo" au ya "kutokukubaliana" au kura ya uamuzi ya aina nyingine yoyote kupigwa, isipokuwa pale ambapo itaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura kwa kufuata wingi wa sauti kwa mujibu wa fasili ya 5 (2) Endapo Spika atasimama wakati wa mjadala, na kuanza kuzungumza, Mbunge yeyote ambaye atakuwa anazungumza wakati huo au ambaye atakuwa amesimama mahali pake akisubiri kuanza kuzungumza, ataketi mahali pake, na Bunge litabaki kimya ili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifa yake. (2) Mbunge aliyedai utaratibu atalazimika kutaja Kanuni au sehemu ya Kanuni ya Bunge iliyokiukwa.

(3) Baada ya kutaja Kanuni au sehemu ya Kanuni ya Bunge iliyokiukwa Mbunge aliyesimama kuhusu utaratibu, ataketi mahali pake kusubiri maelekezo na uamuzi wa Spika.

(4) Spika anaweza, ama papo hapo kutoa uamuzi wake juu ya jambo la utaratibu lililotajwa au kuahirisha uamuzi ili alifikirie zaidi jambo hilo na kutoa uamuzi baadaye au kutoa uamuzi na baadaye kutoa sababu za uamuzi huo, vyovyote atakavyoamua. (2) Kama Spika atakuwa na maoni kwamba kuwasilishwa kwa hoja hiyo ni kinyume cha uendeshaji bora wa shughuli za Bunge, atakataa kuitoa ili iamuliwe; vinginevyo, papo hapo atawahoji Wabunge juu ya hoja hiyo kadri atakavyoona inafaa.

(3) Endapo hoja iliyowasilishwa haitapata kibali cha Bunge, mjadala kuhusu hoja iliyoko mbele ya Bunge utaendelea. (3) Mbunge anayetoa hoja ya kufunga mjadala, anaweza kusimama mahali pake na kutoa hoja "Kwamba mtoa hoja sasa apewe nafasi ya kujibu".

(4) Endapo Spika ataona kuwa hoja ya kufunga mjadala inakiuka mwenendo bora wa Shughuli za Bunge au inavunja haki za Wabunge, basi ataikataa. (2) Mara baada ya kupokea malalamiko yaliyowasilishwa kwake kwa mujibu wa fasili ya (1) (2) Mbunge yeyote aliyehudhuria anaweza kumjulisha Spika kwamba, Wabunge waliopo ni pungufu ya akidi inayohitajika kwa ajili ya shughuli inayoendelea.

(3) Endapo Spika ataridhika kwamba ni kweli idadi ya Wabunge walio ndani ya Ukumbi wa Bunge ni pungufu ya akidi inayohitajika, basi atasimamisha Shughuli za Bunge kwa muda atakaoutaja na atamwagiza Katibu kupiga kengele. (2) Spika, wakati amekalia kiti cha Spika, hatakuwa na kura ya kawaida bali atakuwa na kura ya uamuzi endapo kura za "Ndiyo" na "Siyo" zitalingana.

(3) Wakati mjadala juu ya hoja unapomalizika, Spika atawahoji Wabunge ili kupata uamuzi juu ya hoja hiyo kama ilivyo au baada ya kufanyiwa marekebisho au mabadiliko, Spika kwanza atataka uamuzi wa wale wanaoafiki kwa kusema: "Wale wanaoafiki waseme Ndiyo" na baadaye atataka uamuzi wa Wabunge wasioafiki kwa kusema: "Wale wasioafiki waseme Siyo." Uhalali wa maamuzi ya Bunge Uamuzi wa Bunge (4) Isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo katika Kanuni hizi, uamuzi juu ya mambo yote utapatikana kwa kufuata wingi wa sauti za Wabunge za "Ndiyo" au "Siyo" na Spika atatangaza matokeo ya kura kwa kusema "Naamini Walioafiki Wameshinda" au "Naamini Wasioafiki Wameshinda." (5) Endapo itaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura kwa kufuata wingi wa sauti kwa mujibu wa fasili ya (4) ya Kanuni hii, Spika ataruhusu muda upite ili kutoa nafasi kuhakikisha uamuzi wa Bunge juu ya jambo hilo na kwa muda huo, ikiwa inaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura, Mbunge yeyote anaweza kusimama na kusema "Kura zihesabiwe." (6) Endapo hakuna Mbunge aliyeomba kura zihesabiwe, Spika atatoa kauli ya uamuzi wa mwisho kwa kusema "Walioafiki Wameshinda" au "Wasioafiki Wameshinda", kulingana na hali itakavyokuwa.

(7) Endapo Mbunge yeyote ataomba kura zihesabiwe, basi Spika ataamuru kura zihesabiwe ikiwa Wabunge wengine kumi au zaidi watasimama mara moja kuunga mkono maombi ya kura kuhesabiwa.

(8) Endapo Spika ataamuru kura zihesabiwe, Katibu atapiga kengele ya kuwaita Wabunge kwa muda wa dakika moja na baada ya muda huo, Spika atamwagiza Katibu kumwita Mbunge mmoja mmoja kwa jina lake na kumuuliza anapiga kura yake upande gani na kurekodi kura hiyo.

(9) Bila ya kuathiri masharti ya fasili zilizotangulia za Kanuni hii, Mbunge yeyote atakayepiga kura juu ya jambo lolote ambalo yeye binafsi ana maslahi nalo ya kifedha atahesabiwa kuwa hakupiga kura. (2) Tangazo (2) Kwa mujibu wa wa fasili (1), iwapo tarehe kumi ya mwezi Machi itakuwa si siku ya kazi, uwasilishwaji huo utafanywa tarehe inayofuata ya siku ya kazi.

97.-(1) Tarehe kumi na moja ya mwezi Machi ya kila mwaka au tarehe ya siku nyingine ya kazi inayofuata iwapo tarehe hiyo itakuwa si siku ya kazi, Waziri anayehusika na masuala ya mipango atawasilisha kwa Wabunge, mapendekezo ya Serikali ya mpango kwa mwaka wa fedha unaofuata.

(2) Kwa mujibu wa fasili (1), siku hiyo pia, Waziri anayehusika na masuala ya fedha, atawasilisha kwa Wabunge, mapendekezo ya Serikali ya kiwango na ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha unaofuata.

(3) Katika hatua ya uwasilishwaji wa mujibu wa fasili ya (1) na ya (2), hakutakuwa na mjadala wowote kuhusu mapendekezo ya mpango na kiwango cha ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha unaofuata.

(4) Baada ya mapendekezo ya mpango na kiwango cha ukomo wa Bajeti ya Serikali kuwasilishwa kwa mujibu wa fasili ya (1) na (2) (3) Mbunge atakayeamua kutumia kifungu chenye mshahara wa Waziri, ataruhusiwa tu iwapo ataomba ufafanuzi wa suala mahsusi la sera na hatazungumzia zaidi ya jambo moja. (2) Endapo hoja iliyotolewa kwa ajili ya kupunguza kifungu fulani katika Fungu lolote haijapitishwa, hoja nyingine bado inaweza kutolewa kwa madhumuni ya kupunguza kifungu kingine cha Fungu hilo hilo. (2) Vilevile Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja ya kuondoa shilingi moja katika kifungu chochote cha Fungu hilo.

(3) Madhumuni ya hoja ya aina hiyo ni kumwezesha Mbunge aliyeitoa aweze kueleza kutoridhika kwake na utekelezaji wa jambo fulani mahsusi ambalo dhahiri linahusika na kifungu hicho.

(4) Hoja ya aina hiyo itatolewa kwa muda usiozidi dakika tano.

(5) Wabunge wanaweza kuchangia hoja ya kuondoa shilingi moja iliyoanzishwa kwa mujibu wa fasili ya (2) kwa muda usiozidi dakika tatu kila mmoja.

(6) Waziri anayehusika atapewa nafasi ya kutoa majibu ya hoja hiyo.

(7) Mbunge aliyetoa hoja ya kuondoa shilingi ndiye atakayefunga mjadala wa hoja hiyo. (17) Spika ataweka utaratibu wa kujadili taarifa za Kamati na endapo Kamati yoyote katika kutekeleza majukumu yake, itaona kuwa kuna mambo ya utekelezaji ambayo yanahitaji kurekebishwa, inaweza kutoa taarifa maalumu ya ushauri kwa Waziri mwenye dhamana juu ya mambo hayo ili Waziri aweze kuchukua hatua zinazostahili.

(18) Kamati yoyote inaweza kuunda Kamati Ndogo kwa ajili ya utekelezaji bora wa Shughuli zake, kadri itakavyoona inafaa na kila Kamati Ndogo itapangiwa kazi zake na Kamati ya Kudumu inayohusika.

(19) Mjumbe wa Kamati yoyote hataruhusiwa kuzungumzia au kushughulikia jambo lolote lililofikishwa katika Kamati iwapo ana maslahi binafsi katika jambo hilo au idara hiyo isipokuwa anaweza kufanya hivyo baada ya kutaja jinsi anavyohusika na kiwango cha maslahi hayo. (2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) (2) Akidi ya vikao vya Kamati Teule itakuwa ni theluthi mbili ya wajumbe wake.

(3) Kamati Teule itafanya kikao chake cha kwanza mahali na saa atakayoamua Mwenyekiti na vikao vinginevyo vitafanyika kwa wakati na mahali popote itakapoamua. (2) Taarifa ya Kamati Teule itawasilishwa Bungeni na Mwenyekiti.

(3) Iwapo baada ya hoja kutolewa, Bunge litaamua kujadili taarifa hiyo, hoja itakayotolewa Bungeni itakuwa ni kwa madhumuni ya kuliomba Bunge likubali mapendekezo yaliyomo katika taarifa hiyo.

(4) Bunge linaweza kuamua vinginevyo kwa kutumia utaratibu wa kubadilisha hoja ambao umeelezwa katika Kanuni ya 57 ya Kanuni hizi. (2) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyowekwa saini na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya kuwasilisha hoja hiyo Bungeni yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja kuiwasilisha hoja hiyo Bungeni.

(3) Hoja hiyo itakapowasilishwa Bungeni, Spika atalitaka Bunge, bila ya kufanya majadiliano yoyote, lipige kura ya siri ili kupata uamuzi juu ya hoja hiyo. (2) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyowekwa saini na Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya kuwasilisha hoja hiyo Bungeni yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja kuiwasilisha hoja hiyo Bungeni.

126.-(1) Endapo hoja ya kumshtaki Rais itaungwa mkono na

(3) Hoja hiyo itakapowasilishwa Bungeni, Spika atalitaka Bunge, bila ya kufanya majadiliano yoyote, lipige kura ya siri ili kupata uamuzi juu ya hoja hiyo. (3) Spika atakalia Kiti wakati wa kujadili hoja ya kutaka kumwondoa Naibu Spika madarakani na Naibu Spika atakuwa na haki ya kujitetea wakati wa mjadala.

132.-(1) Endapo hoja ya kumshtaki

(4) Naibu Spika atakuwa ameondolewa kwenye madaraka endapo zitapigwa kura zisizopungua theluthi mbili ya idadi ya Wabunge wote za kuunga mkono hoja hiyo na uamuzi wa Bunge utafanywa kwa kuzingatia kura za siri.

(5) Naibu Spika anayetuhumiwa anaweza kujiuzulu nafasi yake kwa kutoa maelezo ya kujiuzulu kwake Bungeni kabla ya uamuzi juu ya hoja ya kumwondoa madarakani. (2) Mbunge hatapepeza Bendera kwenye gari lake awapo katika Miji ya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar, na anapokuwa anatumia gari la kukodi au la kuazima.

SEHEMU YA KUMI NA TANO

(3) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii, Bendera ya Bunge itapepezwa kuanzia saa 12.00 asubuhi na kuteremshwa mara ifikapo saa 12.00 jioni kila siku. (2) Hoja ya kutengua Kanuni za Bunge haitahitaji kutolewa taarifa.

(3) Maelezo ya hoja ya kutaka kutengua Kanuni yoyote itakuwa ni pamoja na maelezo kuhusu madhumuni ya kutaka Kanuni hiyo itenguliwe.

(4) Kanuni hiyo itatenguliwa kwa madhumuni yaliyokusudiwa tu na siyo kwa madhumuni mengine yoyote.

154.-(1) Endapo litatokea jambo lolote ambalo muhusika wake au mwathirika wa jambo hilo anastahili kupewa pongezi au pole na Wabunge basi Spika atatoa pongezi au pole kwa mhusika au mwathirika wa jambo hilo kwa niaba ya Wabunge wote.

(2) Baada ya Spika kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo lolote, kwa ajili ya kuokoa muda wa majadiliano, Mbunge yeyote hataruhusiwa kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo hilo wakati wowote wa majadiliano Bungeni.

(3) Kwa upande wa Serikali, Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni atatoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo lolote kwa niaba ya Serikali.

(4) Baada ya Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo lolote, kwa ajili ya kuokoa muda wa majadiliano, Waziri yeyote hataruhusiwa kutoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo hilo wakati wowote wa majadiliano Bungeni. (2) Mbunge atapiga kura yake kwa kuweka alama ya "V" katika nafasi wazi ya karatasi ya kura pembeni ya jina la mgombea anayetaka kumpigia. (2) Karatasi ya kura itakataliwa na kura hazitahesabiwa katika karatasi hiyo:-(a) ikiwa karatasi hiyo siyo rangi rasmi ya karatasi ya kupigia kura iliyotolewa na Katibu;

SEHEMU

(b) ikiwa mpiga kura amepiga kura zaidi au pungufu ya zile zinazotakiwa kupigwa;

(c) ikiwa kutaonekana kwenye karatasi hiyo maandishi yoyote au alama yoyote iliyowekwa na mpiga kura isiyokuwa ya ile ya "V";

(d) ikiwa haikuwekwa alama au imewekwa alama isiyoonesha dhahiri ni mgombea yupi ambaye mpiga kura amempigia; isipokuwa kwamba, ikiwa baadhi ya kura kwenye karatasi ya kura ni dhahiri na nyingine si dhahiri, karatasi ya kura Kuhesabu kura Kutangaza matokeo ya kura hiyo itakataliwa kuhusu tu zile kura zisizokuwa dhahiri na kura zilizo dhahiri zitahesabiwa.

(3) Uamuzi wa Spika juu ya kuwa karatasi ya kura ikataliwe yote au sehemu tu utakuwa ni wa mwisho. (2) Endapo baada ya kuhesabu kura kutakuwa na sababu ya kurudia Uchaguzi kutokana na kutokupatikana mshindi katika nafasi yoyote inayohusika katika uchaguzi huo, Spika ataeleza sababu za kutokupatikana mshindi, kisha ataagiza kura ipigwe tena ili kupata mshindi kwa nafasi hiyo.

SEHEMU YA NANE

(3) Kura ya uamuzi haitatumika kwenye uchaguzi.

(4) Iwapo imeamuliwa ipigwe kura tena kwa mujibu wa fasili ya (2), basi wagombea wanaopigiwa kura watakuwa ni wale tu ambao walipata kura sawa. SEHEMU YA TISA UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU ZA KURA 11.-(1) Katibu ataandika maneno "imekataliwa" na "kura iliyokataliwa" kwenye karatasi za kura zilizokataliwa na ataziweka karatasi hizo pamoja na zile zilizokuwa safi kwa muda wa miezi sita baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi.

(2) Baada ya hapo, isipokuwa kama Bunge litaamuru vinginevyo, Katibu ataziharibu karatasi hizo.

(3) Karatasi za kura zilizokwishatumika hazitaonyeshwa kwa mtu yeyote na Katibu, isipokuwa kwa mujibu wa azimio la Bunge baada ya hoja ya kutaka zionyeshwe kupitishwa.

SEHEMU YA KUMI

2.

In these rules, all the parliamentary words and expressions used shall have the same meaning assigned to them in the Parliamentary Standing Orders and, unless the context requires otherwise:-"Candidate" means a person who is nominated to stand for election to the East African Legislative Assembly as provided for in rule 5 of these rules;

"Election" means an election to the East African Legislative Assembly;

"Nomination" means nomination as a candidate to stand for election to the East African Legislative Assembly; "Returning Officer" means the Clerk of the National Assembly; "Treaty" means the Treaty for the Establishment of the East African Community, 1999;

"Voter" means a Member of Parliament present and voting during the election;

In these Rules, unless the context requires otherwise-"Candidate" means a Member of Parliament who is duly nominated to stand for election to the Pan-African Parliament as provided for in rule 5 of these Rules;

"Election" means the election to membership of the Pan-African Parliament;

"Election day" means the day on which the election of Members of the Pan-African Parliament is set to be conducted;

"Nomination" means nomination as a Candidate to stand for election to the Pan-African Parliament; "Nomination day" means the day which shall by notice published by the Returning Officer, be set to be the last day for receiving application forms from Candidates;

"Nominator" means a Member of Parliament of the Parliament of the United Republic of Tanzania entitled to vote, who nominates and supports a Candidate who aspires to stand and contest for election to the Pan-African Parliament;

"Qualification" means the qualification which entitles a person to stand and contest for election to the Pan-African Parliament;

"Returning Officer" means the Clerk of the National Assembly; "Speaker" means the Speaker of the National Assembly; "Voter" means a Member of Parliament of the United Republic of Tanzania present and voting during the election.

PART II QUALIFICATION OF CANDIDATES

3.

A person shall be qualified to be a candidate for election to the East African Legislative Assembly who he is qualified to be elected in accordance with Article 50(2) of the Treaty.

No person shall be qualified to be a Candidate for election to the Pan-African Parliament unless he or she is a Member of Parliament of the United Republic of Tanzania, and is fluent in any of the languages approved for use in the proceedings of the Pan-African Parliament.

PART III NOMINATION OF CANDIDATES

4. -(1) Where an election is to be held, the Returning Officer shall by notice published in the Gazette, appoint a nomination day for that election.

(2) The Returning Officer shall give at least fourteen days notice of such nomination day.

5.-(1)

In order to be validly nominated as a candidate for the East African Legislative Assembly elections, a person must be nominated in a transparent and democratic manner by the political party which is sponsoring him.

(2) The nomination shall be in the prescribed form, signed by the candidate and by the Secretary General of the party nominating him, and shall contain the following particulars:-

The name, educational qualifications, address and occupation of the candidate;

(b) A certificate by the candidate that he is willing and otherwise qualified to stand for election.

(3) Every nomination paper shall be accompanied by the following documents:-

6.

A candidate, or an official of the party nominating him shall, at the time of delivering the nomination paper, deposit a nonrefundable deposit of fifty thousand shillings, to cover for the cost of election expenses.

7.

Objections may be made by the Returning Officer to the nomination of a candidate, if it is apparent to him from the contents of the nomination papers that the candidate is not qualified to stand for election. In which case the Returning Officer shall forthwith reject the nomination papers of that candidate.

PART IV ELECTION AND VOTING PROCEDURE

8. The Returning Officer shall by notice published in the Gazette, appoint an election day which shall be not more than seven days after nomination day, provided that, such election day shall be a day when the National Assembly is sitting in ordinary session.

9.-(1) A candidate may withdraw his candidature by notice in writing, signed and delivered by him to the Returning Officer and a copy to the Secretary General of the Party sponsoring him, not later than four o'clock in the afternoon of the day following nomination day, thereafter no withdraws shall be accepted.

(2) Where any candidate dies after four o'clock in the afternoon of nomination day and before election day, the election process will continue undisturbed.

10.-(1) An aspiring candidate may introduce himself to the voters and seek their support even before nomination day and may continue to do so after nomination day.

(2) Before the votes are cast on election day, each candidate will be permitted to appear before the voters, duly assembled in an ordinary sitting of the House and address them in English for such length of time and answer such number of questions, if any, as may be determined by the Speaker for that purpose. (2) The Returning Officer shall issue only one ballot paper to each voter.

(3) The ballot paper shall contain the names of all candidates, arranged alphabetically in the following groups:- (4) A voter shall be required to cast a specified number of votes, to be announced by the Speaker in each of the groups.

(5) On receiving a ballot paper, each voter shall secretly record his votes by putting a mark against the names of the nine candidates he wishes to vote for. (6) Each voter shall be required to cast as many votes as there are vacancies, otherwise his whole ballot paper will be regarded as spoilt.

(7) A voter who has accidentally spoiled his ballot paper while the voting is still in progress may surrender the spoilt ballot paper to the Returning Officer and obtain a replacement thereof.

12.-(1)

When all the voters have casted their votes, the Speaker shall appoint two counting agents, one from the ruling party and the other from the opposition benches, to act as counting agents for all the candidates.

(2) Immediately after all the ballots have votes been collected, the Returning Officer, with the assistance of Clerk Assistants and before the two counting agents as witnesses, shall count the votes so casted.

(3) In order to enable the National Assembly to proceed with other business, the counting of votes shall take place outside the Assembly Chamber, in a room designated by the Clerk for that purpose within the precincts of the Assembly.

13.

When the votes have already been counted and the results of the election has been ascertained, the Returning Officer shall:-

Report to the Assembly the election results, together with the number of votes recorded for each candidate in each group.

Announce to the Assembly the names of nine persons receiving the majority number of votes in each group and shall declare those persons to have been elected as members of the East African Legislative Assembly.

14.-(1) The Returning Officer shall ensure the safe custody of all ballot papers and other documents relating and pertaining to the conduct of the election.

(2) The Returning Officer shall cause all documents to which this paragraph applies to be destroyed after the expiration of six months from the election day, unless otherwise directed by an order of the High Court arising from any proceedings of a petition relating to the election.

In order to enable the National Assembly to proceed with other business scheduled for that day, the counting of votes shall take place in a room designated by the Speaker for that purpose within the precincts of the Assembly.

PART V ANNULMENT AND AVOIDANCE OF ELECTION

15.

Pursuant to the provisions of Article 52(1) of the Treaty, the election of a candidate as a member of the East African Legislative Assembly may be declared null and void only on an Election Petition.

16. The procedure, jurisdiction and grounds for declaring the election of such member null and void shall be the same as those provided by law for election petitions in respect of Members of the Parliament of the United Republic of Tanzania. (1) If any matter or thing arises which is not specifically provided for in these rules, the Speaker shall make a ruling directing what is to be done in respect of that matter or thing.

(2) In making such a ruling, the Speaker shall be guided by the practices and procedures normally followed in similar situations with regard to Parliamentary elections.

18. These rules may be amended at any time by a resolution of the National Assembly on a proposal submitted to it by the Standing Orders Committee.

Matters not provided for

Amendment of rules 6.-(1) All Tanzania Members of the East African Legislative Assembly shall be present at the time of presentation of any such report.

(2) All such reports shall subsequently be laid on the Table of 1. These Rules may be cited as the Pan-African Parliamentary Election Rules, and shall come into operation on the day of their adoption by resolution of the National Assembly.

PART III NOMINATION PROCEDURE

4.-(1)

Where election of Members of the Pan-African Parliament is to be held, the Returning Officer shall, by written notice circulated to all members of the Parliament of the United Republic of Tanzania, appoint a nomination day for that election, which must be a day during any period when the National Assembly is in ordinary session.

(2) The Returning Officer shall give at least seven days notice of such nomination day.

5.

The following shall be the procedure for the nomination of candidates that:- (a) in the case of a General Election of all the five members of the Pan-African Parliament representing Tanzania, the candidates will be nominated in accordance with the following groups:- (c) in the case of a by-election to fill a casual vacancy, candidates will be nominated only in respect of the group in which the vacancy has occurred;

(d) no candidate may be nominated for more than one specified group.

6.-(1) In order to be validly nominated to stand as a candidate for election to Pan-African Parliament, a person shall be nominated and supported in writing by not less than ten nominators who are entitled to vote at that election. A nominator may nominate up to four candidates, one for each of the four groups.

(2) The nomination shall be in the prescribed form obtainable from the Returning Officer, and shall contain working experience of the candidate.

(3) The time for receipt by the Returning Officer of nomination forms duly completed by the aspiring Candidates shall expire at four o'clock in the afternoon of the nomination day and soon thereafter, the Returning Officer shall give written notification to all Members of Parliament, of the complete list of the all Candidates who have been validly nominated for the election in respect of each of the four groups.

(4) After being validly nominated, a Candidate may withdraw his candidature by notice in writing signed and delivered by him to the Returning Officer, not later than four o'clock in the afternoon of the day following the nomination day, thereafter, no withdrawals shall be accepted.

(5) Where any Candidate dies at any time after nomination day and before election day, the election process shall continue undisturbed.

(6) After being validly nominated, a Candidate may conduct his or her election campaign.

PART IV ELECTION PROCEDURE

7. The Returning Officer shall, by written notice circulated to all Members of Parliament, appoint an election day, which must be a day on which the National Assembly is sitting in ordinary session, and shall be not more than five days after nomination day.

8.

The voting process shall be conducted under the general supervision of the Speaker, provided that, if the Speaker himself or herself is a Candidate, he or she shall vacate the chair before the commencement of the election proceedings.

9.

Before the voting exercise takes place on election day, each Candidate shall be given an opportunity to appear before the voters assembled in an ordinary sitting of the National Assembly and address them in English for such length of time and answer such number of questions, if any, as may be determined by the Speaker for that purpose.

10.

Immediately after address of the candidates, voting shall commence and proceed as follows:-(a)

Only one ballot paper shall be issued to each voter.

(b) The ballot paper shall contain all names of the Candidates arranged in alphabetical order for each of the groups.

(c) Each voter shall be required to cast the exact number of votes equal to the number of persons to be elected in each group. Any ballot be treated as spoilt and will not be counted. (2) A voter who has accidentally spoiled his or her ballot paper while voting is still in progress may surrender the spoilt ballot paper to Returning Officer and obtain a replacement thereof.

12.-(1) Immediately after all the votes have been placed in the ballot boxes and before the ballot boxes are removed from the Assembly Chamber for counting the votes, the Speaker shall appoint one counting agent for the Candidates in each of the groups. Provided that, any candidate who wishes to appoint his or her own counting agent may do so by submitting the name of that agent to the Speaker immediately after the appointments by the Speaker have been announced.

(2) The counting of Votes shall be done by such number of Officers of the Assembly as may be appointed by the Returning Officer, and shall be witnessed by the counting agents.

14.

After the counting of votes is complete and the results ascertained and certified by the Returning Officer and the counting agents, the Returning Officer shall immediately submit the results to the Speaker who shall:-

Report to the Assembly the results of the election together with the number of votes recorded for each candidate in each of the Groups. (2) The Returning Officer shall cause all documents to which this rule applies to be destroyed after the expiration of six months from the election day.

PART V MISCELLANEOUS

16.

Where anything arises which is not specifically provided for in these Rules, the Speaker shall make a ruling directing what is to be done. In making such a ruling, the Speaker shall be guided by the procedures and practices normally followed in similar situations with regard to Parliamentary elections.

17. These Rules may be amended at any time by a resolution of the National Assembly on a proposal submitted to it by the Standing Orders Committee.